Tuesday, July 14, 2009


بِسْمِ اللّهِ الرَّحْمَنِ الرَّحِيمِ

HAKUNA SAUM YAITWA SAUM YA MIIRAJ
Tukio la Miiraj nitukio Asema Allah Alietakasika na akatukuka :-


سُبْحَانَ الَّذِي أَسْرَى بِعَبْدِهِ لَيْلاً مِّنَ الْمَسْجِدِ الْحَرَامِ إِلَى الْمَسْجِدِ الأَقْصَى الَّذِي بَارَكْنَا حَوْلَهُ لِنُرِيَهُ مِنْ آيَاتِنَا إِنَّهُ هُوَ السَّمِيعُ البَصِيرُ
((Ametakasika Aliyemchukua mja Wake usiku mmoja kutoka Msikiti Mtukufu mpaka Msikiti wa Mbali,
ambao Tumevibariki vilivyouzunguka, ili Tumuonyeshe baadhi ya Ishara Zetu. Hakika Yeye ni Mwenye
kusikia na Mwenye kuona))
[Al-Israa: 1]
na ni katika aqida yetu kuiamini hii safari Asema Imaam Abu Ja’afar at-Tahaawi katika kitabu chake
‘Aqeedatu at-Tahaawiyah
Mi'raaj ni kweli, na mtume Salallahu Alaihi Wasallam alichukuluwa katika safari ya al-Israa kiwiliwili chake, akiwa macho na wala sio usingizini hadi mbinguni kisha akapandishwa hadi sehemu aliyopenda Allah, na Allah akamuadhimu Kwake vile Alivyopenda. Na akamfunulia yale aliyotaka kumfunulia (Moyo haukusema uwongo uliyo yaona) [An-Najm:11]. Basi tunamwomba Allah amuenue daraja na amfikishie Rehma na Amani kesho siku ya akhera na kabla ya hapo
LINI LILITOKEA TUKIO HILI:-
Ama kuhusu usiku wenyewe wa tukio hili la Israa na Mi'iraaj hakuna Hadiyth Swahiyh inayoelezea kuwa ilikuwa katika mwezi wa Rajab au tarehe 27 ya mwezi huu wa Rajab kama wengi wanavyodhania. Usimulizi wowote unaotaja mwezi au tarehe ya tukio hili umekosa dalili Swahiyh kama wasemavyo Maulaama wa Hadiyth. Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) kwa hikma Yake Amewafanya watu wasahau siku hii. Hata kama ingelikuwa hiyo siku imetajwa katika dalili basi isingeliruhusiwa Muislamu kuipwekesha kwa kufanya ibada fulani au kusherehekea. Hii kwa sababu Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) wala Maswahaba zake hawakufanya hivyo. Na ingelikuwa kuipwekesha ni amri iliyo katika Dini yetu basi Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) angelitoa mafunzo kwa Ummah wake kwa kauli au vitendo. Na ingelikuwa imefanyika zama zake Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) basi bila shaka ingelijulikana na usimulizi ungelitufikia kwa isnaad Swahiyh kama tulivyopata mafunzo mengineyo ya uhakika

VILE VILE HAKUNA SAUM YA MWEZI WA RAJAB SEMBUSE SAUM YA MIIRAJ


kunapendekezwa mtu kufanya ibada aina yoyote inayoambatana na sheria kwa wingi, katika miezi mitukufu ambao Rajab ni miongoni mwao
Asema Allah:-
( إِنَّ عِدَّةَ الشُّهُورِ عِنْدَ اللَّهِ اثْنَا عَشَرَ شَهْراً فِي كِتَابِ اللَّهِ يَوْمَ خَلَقَ السَّمَاوَاتِ وَالأَرْضَ مِنْهَا أَرْبَعَةٌ حُرُمٌ ذَلِكَ الدِّينُ الْقَيِّمُ فَلا تَظْلِمُوا فِيهِنَّ أَنْفُسَكُمْ ) التوبة/36 , والأشهر الحرم هي : رجب , وذو العقدة , وذو الحجة , والمحرم .
Hakika idadi ya miezi kwa Mwenyezi Mungu ni miezi kumi na mbili katika hukumu ya Mwenyezi Mungu tangu alipo umba mbingu na ardhi. Katika hiyo iko mine mitakatifu. Hiyo ndiyo Dini iliyo sawa. Basi msidhulumu nafsi zenu humo. Na piganeni na washirikina wote kama wao wnavyo pigana nanyi nyote. Na jueni kuwa Mwenyezi Mungu yu pamoja na wachamngu.
Hakika hisabu ya miezi ya kuandama ni miezi kumi na mbili, kwa hukumu na kudra ya Mwenyezi Mungu, na ndivyo alivyo ibainisha katika vitabu vyake tangu kuanza ulimwengu. Na katika hii miezi thinaashara ipo mine imekatazwa kupigana vita ndani yake, nayo:-Mwezi wa Rajab, Alqa'ada (Mfungo Pili), Alhijja (Mfungo Tatu), na Almuharram (Mfungo Nne). Na huku kuitukuza miezi hii mine na kuharimisha kupigana vita ndani yake ndiyo Dini ya Mwenyezi Mungu Iliyo Nyooka, ambayo haibadiliki wala haina mageuzo. Basi msijidhulumu nafsi zenu kwa kuhalalisha vita katika miezi hii, au mkaacha kujilinda adui akikupigeni. Na enyi Waumini! Piganeni na washirikina bila ya kumbagua yeyote kati yao, kama wanavyo kupigeni nyinyi nyote. Na kuweni na yakini kuwa Mwenyezi Mungu atawanusuru wanao mcha, na wakashika amri zake, na wakaepuka anayo yakataza.
WALAKIN HAKUNA MAKHSUS ZA IBADA MAALIM ZA MWEZI WA RAJAB HASWA SAUM

عن خرشة قال: رأيت عمر بن الخطاب يضرب أكف الرجال في صوم رجب حتى يضعونها في الطعام ويقول رجب وما رجب إنما رجب شهر كان يعظمه أهل الجاهلية فلما جاء الإسلام ترك مجمع الزوائد : 3/194
“Nilimuona Umar akiichapa mikono ya wale waliyokuwa wamefunga mwezi wa Rajab mpaka walipofungulia, na alikuwa akisema huu ni mwezi uliyokuwa ukiheshimiwa sana wakati wa jahiliya. (kabla ya Uislamu) Na ulipokuja Uislam Ukaachwa. (Majma'u az-Zawaaid Mj. 3 Uk. 194)(al-Irwaa’, 957; Shaykh Al-Albaaniy kasema ni Sahihi).

قال شيخ الإسلام ابن تيمية رحمه الله في "مجموع الفتاوى" (25/290) :
" وأما صوم رجب بخصوصه فأحاديثه كلها ضعيفة ، بل موضوعة ، لا يعتمد أهل العلم على شيء منها ، وليست من الضعيف الذي يروى في الفضائل ، بل عامتها من الموضوعات المكذوبات

Anasema sheikh Islam Ibnu Taymiyyah :-
Hakika kuifanya saum makhsus kwa mwezi wa Rajab hadith zote ni dhaifu, bali ni maudhui(amesingiziwa Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam)hawazitegemei maulamaa hadithi hizo wala si dhaifu ambazo hutegemewa katika fadhail walakin karibu zote ni maudhui na za urongo....."
مجموع الفتاوى" (25/290)

قال ابن القيم رحمه الله :
" كل حديث في ذكر صيام رجب وصلاة بعض الليالي فيه فهو كذب مفترى " انتهى من "المنار المنيف" (ص96)


Vilevile anasema Sheikh Al Allama Ibnul Qayyim :-
Kila hadith iliotaja kufunga mwezi wa Rajab na kuswali katika baadhi ya usiku wake ni za uorongo na kuzuliwa ("المنار المنيف" (ص96))

وقال الحافظ ابن حجر في "تبيين العجب" (ص11) :
" لم يرد في فضل شهر رجب , ولا في صيامه ولا صيام شيء منه معين , ولا في قيام ليلة مخصوصة فيه حديث صحيح يصلح للحجة " انتهى
.
Na amesema Al Hafidh Ibnul Hajar :-
Haikupokewa katika Fadhla za Rajab wala katika kufunga kitu chochote makhsus(special) wala katika kuswali usiku katika usiku wake swala makhsus katika hadith saheeh ambayo itakuwa ni hoja .."تبيين العجب" (ص11)


وقال الشيخ سيد سابق رحمه الله في "فقه السنة" (1/383) :
" وصيام رجب ليس له فضل زائد على غيره من الشهور , إلا أنه من الأشهر الحرم , ولم يرد في السنة الصحيحة أن للصيام فضيلة بخصوصه , وأن ما جاء في ذلك مما لا ينتهض للاحتجاج به
"
ِAnasema Sheikh Sayyid sabiq :-
Na kufunga Rajab hakuna fadhla zaidi na miezi mengineo, ispokuwa ni mwezi miongoni mwa miezi mitukufu, wala haikupokewa katika hadith sahih ya kwamba katika kufunga rajab kuna fadhla makhsus,na yaliopokewa kwa haya siyakutegemewa kutolewa hoja.فقه السنة" (1/383)

وسئل الشيخ ابن عثيمين رحمه الله عن صيام يوم السابع والعشرين من رجب وقيام ليلته .
فأجاب :
" صيام اليوم السابع العشرين من رجب وقيام ليلته وتخصيص ذلك بدعة , وكل بدعة ضلالة " انتهى .


Na akaulizwa Sheikh Ibnu Uthaimeen Allah amrehemu kuhusu kufunga tarehe 27 ya Mwezi wa Rajab (ijulikanayo kama saum ya Miiraj).
Akajibu:- Kufunga siku ya 27 mwezi wa Rajab nakuhusisha usiku wake kuswali , Ni Bid'a na kila bid'a ni UPOTEVU."مجموع فتاوى ابن عثيمين" (20/
Ewe Muislam zingatia haya:-
Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala):
الْيَوْمَ أَكْمَلْتُ لَكُمْ دِينَكُمْ وَأَتْمَمْتُ عَلَيْكُمْ نِعْمَتِي وَرَضِيتُ لَكُمُ الإِسْلاَمَ دِينً
((Leo Nimekukamilishieni Dini yenu, na nimekutimizieni Neema Yangu, na Nimekupendeleeni UISLAMU uwe ndiyo Dini)) [Al-Maaidah: 3]
Hivyo mwenye kufanya kitendo ambacho hakimo katika Dini yetu itakuwa ni kupoteza muda wake kwa ibada isiyo na thamani kama tulivyoonywa:
من عمل عملاً ليس عليه أمرنا فهو رد البخاري
((Atakayetenda kitendo kisichokuwa chetu (katika dini yetu) basi kitarudishwa)) Al-Bukhaariy

Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) katika khutbah yake mwisho kwenye Hijjatul-widaa' alisema:
يا أيها الناس، ما من شيء يقربكم إلى الجنة ويباعدكم من النار إلا وقد أمرتكم به، وما من شيء يقربكم من النار ويباعدكم من الجنة إلا وقد نهيتكم عنه
((Enyi watu, hakuna jambo lolote ambalo litakukurubisheni na Pepo na kukuepusheni na moto ila nimekuamrisheni nalo. Na hakuna jambo lolote litakalokukurubisheni na moto au kukuepusheni na Pepo ila nimekukatazeni nalo))


Kwa nini Muislamu ajitakie mashaka zaidi ya kufanya ‘Ibaadah isiyokuwa na dalili? Kwa nini kwanza asitimize hizo ambazo tayari dalili zake ziko wazi? Kama Muislamu anapenda sana ‘Ibaadah ya kufunga basi afunge Swawm ya Daawuud lakini wangapi wanaoweza kufanya ‘Ibaadah hiyo?
Juu ya hivyo kufuata bid'ah (uzushi) ni upotofu na kujitakia mtu mwenyewe kuwa na makazi mabaya siku ya Qiyaamah:
إن خير الكلام كلام الله وخير الهدي هدي محمدصلى الله علي وسلم وشر الأمور محدثاتها وكل محدثة بدعة وكل بدعة ضلالة وكلضلالة في النار)) أخرجه مسلم في صحيحه
((Maneno bora ni kitabu cha Allaah (Qur-aan) na uongofu mbora kabisa ni uongofu wa Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) na jambo la shari kabisa ni uzushi, na kila jambo jipya (katika Dini) ni bid'ah (uzushi) na kila bid'ah ni motoni))[Muslim katika Swahiyh yake]
سُبْحـانَكَ اللّهُـمَّ وَبِحَمدِك، أَشْهَـدُ أَنْ لا إِلهَ إِلاّ أَنْتَ أَسْتَغْفِرُكَ وَأَتوبُ إِلَـيْك
Subhaanaka Allaahuumma Wa Bihamdika, Ash-Hadu An Laa Ilaaha Illa Anta, Astaghfiruka Wa Atuubu Ilayka
TUSISAHAU KUWA TUTAULIZWA TULIFANYA NINI KATIKA KUULINGANIA UISLAM

INSHAALLAH TUWE MABALOZI WA UISLAM
Imetayarishwa na
Arms1423@hotmail.com.

Wednesday, July 8, 2009

WAKATI GANI WAKUKUMBATIANA WAKUPIGANA PAMBAJA (HUGING – عانق إ)Haifai Kutoa Mkono Kuamkiana Wanawake na Wanaume

BISMILLAHI RAHMANI RAHEEM



السلام عليكم ورحمة الله وبركاته

وَمَن يُشَاقِقِ الرَّسُولَ مِن بَعْدِ مَا تَبَيَّنَ لَهُ الْهُدَى وَيَتَّبِعْ غَيْرَ سَبِيلِ الْمُؤْمِنِينَ نُوَلِّهِ مَا تَوَلَّى وَنُصْلِهِ جَهَنَّمَ وَسَاءتْ مَصِيرًا
((Na anayempinga Mtume baada ya kumdhihirikia uongofu, na akafuata njia isiyo kuwa ya Waumini, Tutamuelekeza alikoelekea, na Tutamuingiza katika Jahannamu. Na hayo ni marejeo maovu)) [An-Nisaa: 115

Sifa zote njema Anastahiki Allaah Aliyetukuka Mola Mlezi wa walimwengu wote, Swalah na salamu zimshukie kipenzi chetu Mtume Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) na Swahaba zake (Radhiya Allaahu ‘anhum) na watangulizi wema mpaka Siku ya Mwisho.

WAKATI GANI WAKUKUMBATIANA WAKUPIGANA PAMBAJA (HUGING )

Leo imekuwa ni ada na desturi kila tunapokutana kukumbatiana(hug) na haswa baada ya swala ya Idd imekuwa ni kama salamu ya Idd, walakin hebu tuangalie jambo hili Maswahaba walikuwa wakilifanya vipi na sisi tuwaige kwani kuwaiga wao ndio kuongoka kwetu

قال أنس رضي الله عنه : " كان أصحاب النبي صلى الله عليه وسلم إذا تلاقوا ؛ تصافحوا ، فإذا قدموا من سفرٍ ؛ تعانقوا " رواه الطبراني في الأوسط ،ورجاله رجال الصحيح
Walikuwa Masahaba wa Mtume صلى الله عليه وسلم wanapokutana hupeana mikono na wanapotoka safari hukumbatiana (hug)
كما قال المنذري (3/270) ،والهيثمي (8/36) . وروى البيهقي (7/100) بسند صحيح عن الشعبي : " كان أصحاب محمد صلى الله عليه وسلم إذا التقوا ؛ صافحوا ، فإذا قدموا من سفر ؛ عانق بعضهم بعضاً
Walikuwa Masahaba wa Mtume صلى الله عليه وسلم wanapokutana hupeana mikono na wanapotoka safari hukumbatiana (hug) Mmoja wao mwezie


". وروى البخاري في الأدب المفرد (970) ، وأحمد (3/495) عن جابر بن عبد الله قال : " بلغني حديث عن رجلٍ سمعه من رسول الله صلى الله عليه وسلم ، فاشتريت بعيراً ، ثمّ شددتُ عليه رحلي ، فسرتُ إليه شهراً حتى قدمتُ عليه الشام ، فإذا عبد الله بن أنيس ، فقلت للبـواب : قل له : جابر على الباب . فقال : ابن عبد الله ؟ قلتُ : نعم . فخرج يطأ ثوبه فاعتنقني واعتنقته " الحديث . وإسناده حسن كما قال الحافظ ( 1/ 195
..Haifai Kutoa Mkono Kuamkiana Wanawake na Wanaume
عن معقل بن يسار يقول : قال رسول الله صلى الله عليه وسلم : (( لئن يطعن في رأس أحدكم بمخيط من حديد خير له من أن يمس امرأة لا تحل له )) رواه الطبراني في " الكبير الحديث : قال الألباني عنه في " صحيح الجامع : صحيح
Imesimuliwa kutoka kwa Ma’qil ibn Yaassar ambaye amesema kuwa Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa alihi wa sallam) amesema: ((Mmoja wenu kudungwa kichwa kwa sindano ya chuma ni bora kwake kuliko kumgusa mwanamke asiyeruhusiwa kwake)) [At-Twabaraaniy katika Al-Kabiyr na imepewa daraja ya Swahiyh na Shaykh Al-Albaaniy katika Swahiyh Al-Jaami’]


Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema:
“Mwenye kuugusa mkono wa mwanamke bila ya kuwa na uhusiano wa kisheria naye (mahram yake), ataekewa kaa la moto kwenye kitanga chake cha mkono Siku ya Qiyaamah” (Fat-hul Qadiyr).

Mama wa waumini ‘Aaishah (Radhiya Allaahu ‘anha) amesema kuwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alikubali Bay‘ah ya wanawake kwa mdomo tu bila kushikana mikono. Hakika hakugusa mkono wa mwanamke ambaye si mkewe (al-Bukhaariy).


Ni wazi kuwa katika Baiyah ya kwanza, waliyomuahidi kwayo Ma-Answaar waliokuwa wanaume watupu inajulikana katika Siyrah kama Bay‘ah ya kike kwani walitakiwa waahidi kama yale ya wanawake waliokuja baadaye, tofauti yake ni kuwa wanaume walimpatia Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) mikono yao. Allaah Anasema:
“Ewe Nabii! Wanapokujia wanawake walioamini wanakuahidi ya kwamba hawatamshirikisha Allaah na chochote, wala hawataiba, wala hawatazini, wala hawatawaua watoto wao, wala hawataleta uzushi wanaozusha tu wenyewe baina ya mikono na miguu yao, wala hawatakuasi katika jambo jema, basi peana ahadi nao na uwatakie maghfira kwa Allaah. hakika Allaah ni Mwingi wa maghfira, Mwingi wa rehema” (60: 12).
Akasema ‘Aaishah: yeyote katika waumini wanawake aliyekubali hayo na akapasi walipokubali Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) aliwaambia: ((Nendeni kwani mmetimiza kiapo cha utiifu)) Hapana! Naapa kwa Allaah, mkono wa Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) haukugusa mkono wa mwanamke yeyote bali walitoa viapo vyao vya utiifu kwa maneno pekee”. Kisha ‘Aaishah akasema: “Naapa kwa Allaah, Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alipokea viapo vya utiifu kwa njia Aliyoitolea sheria Allaah na mkono wa Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) haujapata kugusa mkono wa mwanamke yeyote. Alipofungamana nao viapo vya utiifu alisema: ((Nimekubali kiapo chako cha utiifu [kwa matamshi])) [Muslim]

Vile vile:
عن أميمة ابنة رقيقة قالت : قال رسول الله صلى الله عليه وسلم : ((إني لا أصافح النساء)) رواه النسائي وابن ماجه وصححه الألباني " صحيح الجامع
Imetoka kwa Umaymah bint Raqiyqah ambaye amesema: “Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Hakika mimi sisalimiani na wanawake kwa kupeana nao mkono) [An-Nasaaiy, Ibn Maajah na imepewa daraja ya Swahiyh na Shaykh Al-Albaaniy katika Swahiyh al-Jaami’]
Tunatumai kuwa dalili hizo zitakuwa ni mafunzo miongoni mwa ndugu zetu ambao wana tabia hii ya kuamkiana kwa mikono na wanaume wasio mahram wao ili wabakie katika radhi za Mola wao na pia kuepukana na madhara yake.

((وَمَا آتَاكُمُ الرَّسُولُ فَخُذُوهُ وَمَا نَهَاكُمْ عَنْهُ فَانتَهُوا))
((Na anachokupeni Mtume chukueni, na anacho kukatazeni jiepusheni nacho)) [Al-Hashr: 7]

Wa Allaahu A'alam
سُبْحـانَكَ اللّهُـمَّ وَبِحَمدِك، أَشْهَـدُ أَنْ لا إِلهَ إِلاّ أَنْتَ أَسْتَغْفِرُكَ وَأَتوبُ إِلَـيْكSubhaanaka Allaahuumma Wa Bihamdika, Ash-Hadu An Laa Ilaaha Illa Anta, Astaghfiruka Wa Atuubu Ilayka
TUSISAHAU KUWA TUTAULIZWA TULIFANYA NINI KATIKA KUULINGANIA UISLAM
IMETAYARISHWA NA ABUDUJANA arms1423@hotmail.com
Usinisahau kwenye dua zako
INSHAALLAH TUWE MABALOZI WA UISLAM